Wednesday, June 29, 2011

KAZI ZA WANAFUNZI: KITABU CHA UFUNUO WA YOHANA


SWALI: ONYESHA UHALISI WA LUGHA ISHARA ZILIZOTUMIKA              KUELEZEA IMANI YA  KIKRISTO KUPITIA  KWA BARUA SABA KWA    MAKAN  IS A  SABA.


MAPITO YA IMANI

Katika mapito ya imani mara nyingi kanisa linakumbana na changamoto mbalimbali  kama tulinyoona katika makanisa saba[2]  yalinyoweza kukumbana na changamoto za mafundisho ya uongo  yaliopelekea kupotosha  imani zao na kugeukia mafundisho haya yasiyokuwa ya imani itokayo kwa Mungu[3] . Kwa hali hiyo barua hizo ziliwatia moyo  na kuwa faraja kwao kutokana na majeraha  waliyoyapata  kupitia mafundisho ya uongo kwa kipindi  hicho wakristo wengi  walijeruhiwa.
                        

HATUA  ZA IMANI

Katika makanisa  haya saba  kwa barua hizo ziliwakumbusha kumrudia Mungu wao na kuona ukweli wa neno la Mungu, kuwa wanatakiwa  kutazama  nyuma na kuangalia mbele  na waishi sasa (Uf 2:5)[4]


Tunachojifunza  kuhusu barua za makanisa  saba  yaliyopo katika kitabu cha ufunuo ni UVUMILIVU  NA UNYENYEKEVU[5], katika imani na kujenga imani iliyo dhabiti  katika uwepo wa Mungu  na kuwa na tumaini la uzima wa milee.Katika  barua hizi tunakumbushwa kutazama  nyuma  kuangalia mbele  na kuishi sasa.





MAONI YA MKUFUNZI:
WAHUSIKA WA KIKUNDI

  1. YOHANA KALIKI
  2. CELESTINE  RABANI
  3. NEEMA  ANDREA
  4. MARKO BUNKWIMBA
  5. DANIEL  OPUDO


[1] Hakuna utangulizi unaofanana na hitaji la swali (alama
[2] Mlitakiwa kujadili kwa kina ishara na lugha mbali mbali katika kifungu cha maandiko mlichopewa. Tofauti yake mnatoa taarifa ya nini mlichofundishwa.
[3] Ni sawa, lakini unapopewa kazi ya insha, tafadhali tambua wapi pa kuandika nini. Wazo hilo lilitakiwa kuwa kwenye hitimisho.
[4]  Katika sehemu (aya) hii mmejaribu kukusanya mawazo yote na kuandika kwa ufupi. Lengo la kazi hii haikuwa na kusudi hilo. Ulitakiwa kueleza lugha za ishara zote zinazo patikana katika barua za makanisa yote saba na kisha kujibu kwa namna gani imani ya kikristo inanufaika na barua hizo hasa katika ulimwengu wa sasa.
[5] Haya ni baadhi tu ya mafundisho ya kikristo yapatikanayo katika barua hizo. Kuna mafundisho mengine kama Upendo, Kutoshikamana na dhambi, Kutenda haki nk.

MAONI YA UJUMLA:
Kazi hii siyo ya kitaaluma: Mlitakiwa kuonyesha kwa ufupi lengo la barua, lugha au ishara zinazotumiwa na mwandishi kisha kuziweka bayana ufaidishaji katika kanisa leo.

No comments:

Post a Comment